Local News
Dkt Gwajima Watakao Sababisha Vifo Kushitakiwa
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt.Dorothy Gwajima amewagiza Waganga Wakuu wa Mikoa kuhakikisha wanatoa taarifa za vifo vinavyotokea kwenye maeneo yao kwa lengo la kuiwezesha Kamati ya Kitaifa ya Ufuatiliaji kutathimini kama vifo hivyo vimesababishwa na uzembe wa kutowajibika ipasavyo wakati wa kutoa huduma ili waliohusika na uzembe huo wawajibishwe kwa mujibu wa sheria kupitia mabaraza ya kitaaluma.
Agizo hilo amelitoa Jijini Dodoma alipotembelea Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Dodoma katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa mpango mkakati wa miaka mitano wa Sekta ya afya uliozinduliwa Julai 2021 eneo la kipaumbele cha kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi ambavyo vimeendelea kuwa changamoto. Dkt. Gwajima amesema tafiti zinaonyesha vifo vitokanavyo na uzazi vinazuilika na pia Serikali inafanya jitihada za kusogeza huduma kwa jamii lakini bado kasi ya kupunguza vifo hivyo hairidhishi.
Dkt.Gwajima amesema kuwa, ili kukabiliana na hali hiyo Wizara ya Afya kuanzia tarehe 20 Desemba 2021 itaanza kufanya vikao vya ufuatiliaji kwa njia ya mikutano kupitia mitandao kwa kuunganisha Kamati za Wizara, Mikoa na Watendaji waliopo kwenye vituo kilipotokea kifo husika ndani ya saa 24 kwa lengo la kubaini kama kifo hicho kingeweza kuzuilika ili kama kuna uzembe wa kutowajibika ipasavyo, wahusika wafikishwe kwenye vyombo vya kisheria vya taaluma yao.
Akizungumza kwa niaba ya Waganga Wafawidhi wa hospitali za mikoa hapa nchini, Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Dodoma Dodoma Dkt. Ibenzi Ernest ameahidi kupitia umoja wao watahakikisha wanasimamia kikamilifu utoaji wa huduma bora ili kupunguza vifo vya uzazi visitokee ikiwemo kutoa elimu kwa jamii kuwahi kwenye vituo vya kutoa huduma za Afya wakati wa kujifungua huku wananchi wakipongeza serikali kwa kuboresha huduma za Afya.
v
DC MTWARA APOKEA VIFAA VYA UJENZI WA CHUJIO
Mkuu wa wilaya ya Mtwara Dunstan Kyobya ameongoza zoezi la upokeaji wa vifaa vya ujenzi wa chujio la maji.
Chujio hilo ambalo linajengwa Mangamba iliyoko Manispaa ya Mtwara Mikindani, kukamilika kwake linatarajia kuondoa adha ya uchagu wa maji ambayo wanaipata wakazi wanufaika na mradi huo.
Akizungumza jana wakati wa kupokea vifaa hivyo mkuu wa wilaya huyo amesema kuwa amesikitishwa na mzabuni wa mchanga kwa kuto timiza majukumu yake vema, na kumtaka ndani ya wiki mbili awe amepeleka mchanga huo kutoka nchini Uturuki.
Watu 1.2 milioni wachanjwa chanjo ya Uviko-19
Serikali ya Tanzania imesema hadi kufikia Desemba 18,2021 watu zaidi ya 1.2 milioni wamechanjwa na kupata kinga kamili dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19.
Hayo yamesemwa leo Jumapili Desemba 19,2021 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Profesa Abel Makubi.
Amesema lengo ni kufikia asilimia 60 ya wananchi wote ambayo ni sawa na watu milioni 35.
Profesa Makubi amesema mwitikio wa watu kuchanja sio wa kusuasua ukilinganisha na nchi nyingine.
Amesema kilichochangia watu wengi kutojitokeza ni taarifa potofu zilizoanza kutolewa na makundi mbalimbali ya kijamii kuhusu chanjo hiyo wakati suala la chanjo lipo nchini kwa zaidi ya miaka 100 sasa.
“Imetuchukua muda kuwaelimisha wananchi ili tuwaondolee hayo mashaka. Natumaini sasa wananchi wametuelewa, elimu inatolewa na kesho yake wanachanja,”amesema.
Aidha, Profesa Makubi amesema Desemba 22,2021 watafanya uzinduzi wa kampeni-jamii shirikishi ya pili dhidi ya afua na kinga ya Uviko-19 jijini Arusha.
Amesema ili kufanikisha malengo ya awamu ya pili na matumizi ya watoa huduma ngazi ya jamii, Wizara na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imeandaa mwongozo wa wawezeshaji wa wahudumu wa afya ya jamii.
TANDAHIMBA: DAKTARI AKAMATWA AKIFANYA UPASUAJI NYUMBANI
Daktari mmoja aliyejulikana kwa jina la KARIM BAKARI kutoka kijiji cha Maheha wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara anashikiliwa na jeshi la polisi wilayani humo kwa kosa la kutoa huduma za upasuaji na matibabu kwa wagonjwa nyumbani kwake kinyume na taratibu.
Daktari huyo ambaye alifukuzwa kazi mwaka jana katika hospitali ya wilaya ya Newala kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mgongwa aliyefanyiwa upasuaji amesema aliamua kufanya hivyo kutokana na msongo wa mawazo aliokuwa nao na kuomba serikali imsamehe.
Amesema anajua kwamba amefanya kosa kubwa la kisheria la kutoa huduma nyumbani kwake na kuhatarisha maisha ya wananchi anaowapatia huduma jambo ambalo ni hatari
Mkuu wa wilaya ya Tandahimba Kanali PATRICK SAWALA amesema kukamatwa kwa daktari huyo ni kutokana na uchunguzi uliofanywa kwa muda mrefu baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi.
Kanali Sawala ameliagiza sheji la Polisi wilayani humo kufuata hatua za kisheria na kufuatilia kwa kina wapi ambako alikuwa akipata dawa na vifaa tiba ambavyo vilikuwa vinatumika wakati anatoa huduma nyumbani kwake huki akionya wale wanaoendelea kufanya hivyo katika wilaya yake kuacha mara moja.
Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa wilaya ya Tandahimba Daktari SILAS SEMBIKO amewataka wananchi kuacha tabia ya kupata huduma za afya vichochoroni kwani ni hatari kwa afya zao.
MNADA WA PILI WA KOROSHO BEI YA JUU 2401 KILO

Mnada huo wa pili wa mauzo ya korosho umefanyika katika MATOGORO AMCOS Tandahimba ambapo korosho zilizo uzwa ni kutoka Ghala la TANECU Tandahimba na Newala kutoka kwa Chama Kikuu cha Ushirika cha Tanecu.
Wakulima hao wamesema Mnada umeanza kwa bei nzuri hivyo hawaoni sababu ya kuacha kuuza korosho zao.
Mnada huo umehudhuriwa na mkuu wa wilaya ya Tandahimba Kanali Patrick Sawala ambaye amewataka viongozi wa vyama vya ushirika kusimamia ubora wa korosho zinazo letwa maghalani ili kudhibiti ubora wa Korosho.
Kanali Patrick Sawala amesititiza kuwa serikali haita mvumilia mkulima yoyote atakae changanya kurosho safi na chafu kwani kufanya hivo ni kinyume cha sheria.
Mnada wa tatu wa korosho kutoka Chama Kikuu cha Ushirika cha Tanecu unatarajia kufanyika Kitangali. Oktoba 23 mwaka huu katika wilaya ya Newala mkoani Mtwara.
DC TUNDURU AKAMATA KOROSHO MBOVU
Mh.Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Bw. Julius Mtatiro amekamata zaidi ya tani kumi za korosho Chafu ambazo zimeingia Wilaya ya Tunduru kutoka Wilaya na Mikoa ya Jirani ambapo korosho hizo zingefanikiwa kuuzwa zingeongeza kushuka kwa ubora wa korosho za Tunduru.
WAZIRI MKUU "MSD NATOA WIKI MOJA MUWE MUMESAMBAZA DAWA
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) Meja Jenerali Gabriel Saul Mhidze ahakikishe mpaka kufikia Jumamosi, Oktoba 16, 2021 dawa ziwe zimepatikana katika maeneo yote nchini.
Waziri Mkuu amesema kuwa ni maelekezo ya Serikali kuwa vituo vyote vya kutolea huduma zikiwamo zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya, hospitali za rufaa za mikoa lazima zipate dawa kwa kuwa zinategemea MSD
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Oktoba 10, 2021) alipokutana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Meja Jenerali Gabriel Saul Mhidze, Jijini Dodoma
Pia, Waziri Mkuu amewataka viongozi wa Taasisi hiyo wahakikishe wanapeleka malori 10 ya dawa katika kila kanda lengo ni kuwezesa upatikanaji wa dawa ili kurahisisha utoaji wa huduma.
Page 1 of 184